Skip to main content

Harmonize afunguka haya kuhusu H Baba kumkingia kifua na kujibizana na watu mitandaoni kisa yeye

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Harmonize ameweka wazi kuhusu kile anachokifanya msanii mwenzake wa Bongo Fleva ambaye pia yupo kwenye lebo ya Konde Gang H Baba kuonekana kumkingia kifua sana Harmonize na kufikia hatu hata kuwaongelea watu wengi na kuwakemea pale anapoona wanamuongelea au kumpiga vita Harmonize.

Harmonize ameongea hayo akifanya mahojiano na kituo cha east Afrika Redio na majibu ya Harmonize yalikuwa hivi:”H Baba ni mmoja ya kaka zangu ambaye alinitangulia kwenye sanaa lakini suala na kupost na kufanya nini sijui huwezi kumpangia mtu maamuzi yake ile ni akaunti yake na anachokizungumza anazungumza kitu anachoona yeye kwake ni sahihi, Sasa ukitaka kumpangia mtu kwamba usipost hiki utakuwa kama unamuingilia maisha yake halafu ukiangalia mi mdogo tu nimeanza sanaa juzi tu, Itaonekana mdogo wangu we unanifundisha unajua mi nimepitia machungu mangapi?, Kwahiyo ni mtu ambaye namheshimu na nayaona anayepost kama unavyoona wewe”

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji watatu PSG wakutwa na corona

  Mshambuliaji wa timu ya Paris Saint-Germain,  Neymar de Santos,   ameripotiwa kukutwa na virusi vya corona pamoja na wachezaji wengine watatu. Hata hivyo  Paris Saint-Germain  ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Ufaransa na kumaliza nafasi ya pili kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, wameshindwa kuwaweka wazi wachezaji hao wengine ambao wamekutwa na virusi hivyo. Lakini  Angel Di Maria  mwenye umri wa miaka 32 na Leandro Paredes mwenye miaka 26, wanatajwa kuwa kati ya wachezaji hao kwa mujibu wa L’Equipe. Mara baada ya Paris Saint-Germain kumaliza mchezo wa mwisho wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich, Agosti 23, wachezaji hao watatu walionekana kuwa pamoja kwenye visiwa vya Ibiza wakiponda raha ambapo ni Neymar, Di Maria na Paredes.

MWONGOZO WA USAFIRISHAJI WA BIDHAA MUHIMU NA HUDUMA KATIKA NCHI ZA SADC KWA KIPINDI HIKI CHA JANGA LA VIRUSI VYA CORONA

Tarehe 6 Aprili, 2020 ulifanyika Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).  Mkutano huo ulijadili janga la mlipuko wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu (COVID-19) unaosababishwa na virusi vya Corona. Mkutano huo ulihusisha Mawaziri wenye dhamana ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Fedha,Viwanda,Biashara, Utalii, Mambo ya Ndani na Uchukuzi, kutoka nchi 16 wanachama wa SADC ambazo ni Angola, Botswana, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Namibia, Jamhuri ya Visiwa vya Ushelisheli, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Zambia. Katika mkutano huo, Baraza la Mawaziri lilitoa mwongozo kuhusu Usafirishaji wa Bidhaa Muhimu na Huduma Katika Nchi za SADC katika kipindi hiki cha janga la Virusi vya Corona.  Mwongozo huu utatumika katika kipindi hiki unalenga kupunguza safari zisizo za lazima na usafirishaji wa bidhaa ambazo ni za muhimu tu na unazitaka Nchi Wanachama kuzingatia na kutekeleza sera na miongozo mbalimbali

Mambo muhimu ya kuzingatia unapohitaji kufanikiwa

Wengi wetu mara nyingi huwa tunafikiri kukosa mafanikio ni matokeo ya kukosa bahati katika maisha. Fikra hizo mara nyingi, huwazuia  wengi katika kufanikiwa na kujikuta wakiishia kuwa  watu wa kulaumu na kushindwa kila siku. Kimsingi  kitu kikubwa kinachochangia kuzuia mafanikio yetu ni baadhi ya tabia tulizo nazo. Si kweli kwamba watu wengi hushindwa kuendelea kutokana na kukosa mitaji bali ni kwa sababu ya tabia zao. Tabia ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya mtu binafsi kuliko unavyodhani. Zingatia haya yafuatayo ikiwa unahitaji kufanikiwa katika maisha yako:- Epuka kufikiria sana juu ya makosa uliyoyafanya. Kama kuna sehemu ulikosea katika siku za nyuma, hiyo imeshapita chukua hatu za kusonga mbele. Acha kutumia muda wako mwingi na kufikiri pale ulipokosea kwani hiyo haitakusaidia zaidi ya kukurudisha nyuma. Kumbuka kuwa kukosea ni sehemu ya maisha ya binadamu, kitu cha msingi jifunze kutokana na hayo makosa. Usiwe mtu wa kuongelea ndoto zako kila siku. Wengi