Skip to main content

Posts

Showing posts from 2020

Wachezaji watatu PSG wakutwa na corona

  Mshambuliaji wa timu ya Paris Saint-Germain,  Neymar de Santos,   ameripotiwa kukutwa na virusi vya corona pamoja na wachezaji wengine watatu. Hata hivyo  Paris Saint-Germain  ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Ufaransa na kumaliza nafasi ya pili kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, wameshindwa kuwaweka wazi wachezaji hao wengine ambao wamekutwa na virusi hivyo. Lakini  Angel Di Maria  mwenye umri wa miaka 32 na Leandro Paredes mwenye miaka 26, wanatajwa kuwa kati ya wachezaji hao kwa mujibu wa L’Equipe. Mara baada ya Paris Saint-Germain kumaliza mchezo wa mwisho wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich, Agosti 23, wachezaji hao watatu walionekana kuwa pamoja kwenye visiwa vya Ibiza wakiponda raha ambapo ni Neymar, Di Maria na Paredes.

HIZI HAPA FAIDA ZA KULA TANGO

Matango yanashika nafasi ya nne kwa kulimwa katika aina ya mbogamboga zinazolimwa duniani kote na tunda hili linafahamika kuwa miongoni mwa vyakula bora kwa afya yako maranyingi yanaitwa superfood. JINSI YA KUCHAGUA TANGO BORA KWA AFYA YAKO 1.Angalia tango lenye rangi ya kijani mkozo(dark green) 2.Angalia tango ambalo bado ni ligumu vizuri halijalegea(firm). Baada ya kuchagua tango osha vizuri kwa maii safi sasa unaweza kulitumia kwenye kachumbari,au kwa kulikata na kula hivyovyo,pia kutengenezea juisi FAIDA ZA KUTUMIA MATANGO 1.Kuupatia mwili maji ya kutosha Kwa wale ambao ni wavivu au wako busy sana hata kupata muda wa kunywa maji ya kutosha inakuwa ngumu,Tafuta matango ya baridi ambayo asilimia tisini ni maji,Yatasaidia kurudisha maji yaliyopotea mwilini 2.Husaidia kupambana na joto kali ndani na nje ya mwili Kula tango husaidia kupunguza joto kali ndani ya mwili(heartburn) na pia kupaka kwenye ngozi kutakusaidia kpunguza kuungua na jua 3.Huondoa sumu mwilini(toxins

MWONGOZO WA USAFIRISHAJI WA BIDHAA MUHIMU NA HUDUMA KATIKA NCHI ZA SADC KWA KIPINDI HIKI CHA JANGA LA VIRUSI VYA CORONA

Tarehe 6 Aprili, 2020 ulifanyika Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).  Mkutano huo ulijadili janga la mlipuko wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu (COVID-19) unaosababishwa na virusi vya Corona. Mkutano huo ulihusisha Mawaziri wenye dhamana ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Fedha,Viwanda,Biashara, Utalii, Mambo ya Ndani na Uchukuzi, kutoka nchi 16 wanachama wa SADC ambazo ni Angola, Botswana, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Namibia, Jamhuri ya Visiwa vya Ushelisheli, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Zambia. Katika mkutano huo, Baraza la Mawaziri lilitoa mwongozo kuhusu Usafirishaji wa Bidhaa Muhimu na Huduma Katika Nchi za SADC katika kipindi hiki cha janga la Virusi vya Corona.  Mwongozo huu utatumika katika kipindi hiki unalenga kupunguza safari zisizo za lazima na usafirishaji wa bidhaa ambazo ni za muhimu tu na unazitaka Nchi Wanachama kuzingatia na kutekeleza sera na miongozo mbalimbali

Mambo muhimu ya kuzingatia unapohitaji kufanikiwa

Wengi wetu mara nyingi huwa tunafikiri kukosa mafanikio ni matokeo ya kukosa bahati katika maisha. Fikra hizo mara nyingi, huwazuia  wengi katika kufanikiwa na kujikuta wakiishia kuwa  watu wa kulaumu na kushindwa kila siku. Kimsingi  kitu kikubwa kinachochangia kuzuia mafanikio yetu ni baadhi ya tabia tulizo nazo. Si kweli kwamba watu wengi hushindwa kuendelea kutokana na kukosa mitaji bali ni kwa sababu ya tabia zao. Tabia ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya mtu binafsi kuliko unavyodhani. Zingatia haya yafuatayo ikiwa unahitaji kufanikiwa katika maisha yako:- Epuka kufikiria sana juu ya makosa uliyoyafanya. Kama kuna sehemu ulikosea katika siku za nyuma, hiyo imeshapita chukua hatu za kusonga mbele. Acha kutumia muda wako mwingi na kufikiri pale ulipokosea kwani hiyo haitakusaidia zaidi ya kukurudisha nyuma. Kumbuka kuwa kukosea ni sehemu ya maisha ya binadamu, kitu cha msingi jifunze kutokana na hayo makosa. Usiwe mtu wa kuongelea ndoto zako kila siku. Wengi

Mchezaji wa Yanga aliesaini mkataba mpya wa miaka miwili

Mchezaji wa Yanga Bernald Morson Ameongeza Mkataba wa miaka miwili kuendelea kuwatumikia mabingwa wakihistoria kutoka Jangwani. Morson amesaini mkataba huo chini ya udhamini wa Kampuni ya GSM

Harmonize afunguka haya kuhusu H Baba kumkingia kifua na kujibizana na watu mitandaoni kisa yeye

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Harmonize ameweka wazi kuhusu kile anachokifanya msanii mwenzake wa Bongo Fleva ambaye pia yupo kwenye lebo ya Konde Gang H Baba kuonekana kumkingia kifua sana Harmonize na kufikia hatu hata kuwaongelea watu wengi na kuwakemea pale anapoona wanamuongelea au kumpiga vita Harmonize. Harmonize ameongea hayo akifanya mahojiano na kituo cha east Afrika Redio na majibu ya Harmonize yalikuwa hivi:”H Baba ni mmoja ya kaka zangu ambaye alinitangulia kwenye sanaa lakini suala na kupost na kufanya nini sijui huwezi kumpangia mtu maamuzi yake ile ni akaunti yake na anachokizungumza anazungumza kitu anachoona yeye kwake ni sahihi, Sasa ukitaka kumpangia mtu kwamba usipost hiki utakuwa kama unamuingilia maisha yake halafu ukiangalia mi mdogo tu nimeanza sanaa juzi tu, Itaonekana mdogo wangu we unanifundisha unajua mi nimepitia machungu mangapi?, Kwahiyo ni mtu ambaye namheshimu na nayaona anayepost kama unavyoona wewe”

Ujio mpya wa Chid Benz balaa, Akutana na Naibu Waziri wa Habari Shonza kuomba baraka na kuzungumza haya

Msanii wa bongofleva nchini Rashid Abdallah maarufu kama Chid Benz amemweleza Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza kuwa mapema wiki ijayo anatarajia kutoa video ya wimbo wake wa Beautiful na pia atatunga wimbo wa kuhusu Corona katika kikao kilichofanyika leo jijini Dodoma. Waziri Shonza amemhakikishia Chid Benz kuwa wizara ipo tayari kumpa ushirikiano wakati wowote na kikubwa ni msanii huyo kujituma na kuonyesha umma kwamba kweli ameachana na matumizi ya madawa ya kulevya.

Mwalimu chupuchupu kuuawa na wananchi, wenzake wamnusuru kwa kumfungia na kufuli ofisini

Mwalimu wa Shule ya Msingi Mitonji katika Kijiji cha Mitonji Kata ya Mbuyuni katika Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara, John Mandanda amenusurika kuuawa na wananchi wenye hasira kali, baada ya kuwacharaza viboko wanafunzi hadi mmoja kupoteza fahamu. Mwanafunzi huyo wa darasa la sita (jina linahifadhiwa) anadaiwa kupoteza fahamu kwa zaidi ya saa moja. Kutokana na tishio la kuchapwa na wananchi hao walimu walimwokoa mwenzao kwa kumfungia ndani ya ofisi, huku wananchi hao waliotaka kumpa kichapo wakiwa wamebeba marungu, mashoka na silaa zingine za jadi. Akizungumza na Nipashe jana kwa njia ya simu, Ofisa Elimu Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Elizabeth Mlaponi, alisema mwalimu huyo alifanya tukio hilo juzi majira ya saa 5:00 asubuhi wakati wanafunzi walipokuwa wakiingia darasani baada ya mapumziko mafupi. Alisema mwalimu huyo akiwa shuleni hapo siku ya tukio, alitoa adhabu kwa baadhi ya wanafunzi ambao inaelezwa kuwa wanafunzi hao walikuwa wamechelewa kuingia darasani

Lukaku aeleza alivyokataa ombi la Solskjaer la kubaki Man United

Mshambuliaji wa zamani wa Man United anayeichezea club ya  Inter Milan ya Italia Romelu Lukaku ameweka wazi kuwa kocha wa Man United Ole Gunnar Solskjaer alimtaka asiondoke katika club hiyo ili aendelee kuitumikia Man United. “Ilikuwa ni hali ngumu kwangu na nilitakiwa nifanye maamuzi ya kwenda sehemu ambayo naweza kujifunza vitu vingine kuhusiana na uchezaji wangu na kufanya kazi na mtu ambaye ananihitaji, Ole alinitaka nibaki lakini nilimwambia kuwa nimemaliza”>>> Lukaku Lukaku aliondoka  Man United 2019 baada ya kukaa katika club hiyo kwa miaka miwili lakini hakuwa na wakati mzuri sana kama ilivyokuwa kwa Inter Milan, Lukaku aliishawishi Man United imsajili 2017 kufuatia kiwango chake cha kucheka na nyavu alichokionesha Everton lakini ikawa tofauti akiwa Man United.